Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 4 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 27 2018-04-06

Name

Amina Nassoro Makilagi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA N. MAKILAGI aliuliza:-
Zipo sheria nyingi ambazo zimepitwa na wakati na sheria nyingine ni kikwazo katika kufanikisha shughuli muhimu za Taifa letu.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuzitambua sheria zote zilizopitwa na wakati na zile zinazochelewesha ukuaji wa uchumi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria napenda kujibu swali la Mheshimiwa Amina Nassor Makilagi, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali wakati wote imekuwa na mkakati wa kuhakikisha kwamba sheria zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinapitiwa na kufanyiwa marekebisho kadri inavyohitajika ili kukidhi mahitaji. Mkakati huo unasimamiwa na Wizara kupitia Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania iliyoanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria, Sura ya 171. Tume hii ni chombo mahsusi cha Serikali chenye kazi ya kusimamia mpango huo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu kuanzishwa kwake mwaka 1983, Tume ya Kurekebisha Sheria imefanikiwa kuandaa ripoti 37 za mapitio na marekebisho ya sheria mbalimbali na kuziwasilisha Serikalini ambapo baadhi yake zilishatungiwa sheria na nyingine zinaendelea kufanyiwa kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya mapitio ya sheria ili kubaini sheria zilizopitwa na wakati na hatimaye kupendekeza marekebisho, kutunga sheria mpya au kufutwa kwa sheria ni endelevu na imekuwa ikifanyika muda wote ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika nchi yetu.