Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 4 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 26 2018-04-06

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa (ambulance) kwenye Hospitali ya Wilaya ya Handeni hasa ikizingatiwa hospitali hiyo inahudumia wagonjwa wengi kutoka takribani majimbo manne?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Omari Abdallah Kigoda Mbunge wa handeni kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Mji Handeni ina gari moja la wagonjwa lenye namba za usajili SM 11322 ambalo linatoa huduma kwa wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni. Gari hilo kwa sasa liko katika matengenezo Mjini Tanga baada ya kupata hitilafu. Taratibu za matengenezo zinaendelea kufanyika ili liendelee kutoa huduma kwa wagonjwa. Katika hali ya dharura, Halmashauri inatumia magari ya kawaida kutoa huduma kwa wagonjwa hadi hapo gari la wagonjwa litakapotengemaa.