Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 44 2018-04-10

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Vituo vya Afya Kata za Mtwango, Mninga na Makungu?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea na ujenzi wa vituo vya afya awamu kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha. Katika mwaka wa fedha 2017/2018 kipaumbele kimewekwa katika ujenzi wa Kituo cha Afya Malangali kilichoko katika Jimbo la Mufindi Kusini ambao unahusisha ujenzi wa jengo la upasuaji, nyumba ya watumishi, maabara na jengo la wazazi kwa gharama ya shilingi milioni 400 ili kukiwezesha kutoa huduma za dharura za upasuaji.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2018/2019 Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imetenga jumla ya shilingi milioni 40 kwa ajili ya umaliziaji wa Kituo cha Afya cha Mninga. Fedha hizo zinatarajiwa kufanya umaliziaji wa jengo la wagonjwa wa nje (OPD) ambapo itatumika kiasi cha shilingi milioni 30 na shilingi milioni 10 za kuanzia ujenzi wa nyumba ya mganga.
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa Vituo vya Afya Mtwango na Mninga umefikia hatua mbalimbali ambapo majengo ya maabara na nyumba ya mtumishi imefika hatua ya umaliziaji na vifaa vyote vya umaliziaji vimekwishafika site. Majengo ya upasuaji na akina mama yamefikia hatua ya kunyanyua kuta na vifaa vyote vya ukamilishaji vipo site, tunategemea kukamilisha kabla ya tarehe 31 Mei, kwa mujibu wa mkataba.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Kata ya Makungu hakuna ujenzi unaoendelea isipokuwa kuna kituo cha afya kinachomilikiwa na Kiwanda cha Karatasi cha Mgololo. Katika kituo hicho Serikali imepeleka Watumishi ambao wanalipwa mishahara na stahili zote kutoka Serikalini na kuchangia dawa pamoja na vifaa.