Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 6 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 51 2018-04-10

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. JUMA S. NKAMIA aliuliza:-
Wilaya ya Chemba haina Kituo cha Polisi; je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Kituo cha Polisi na nyumba za askari?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Juma Nkamia, Mbunge wa Chemba, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa Jeshi la Polisi lina uhaba wa vituo vya polisi pamoja na nyumba za kuishi Askari kote nchini ikiwemo Wilaya ya Chemba. Ili kutatua changamoto hii Jeshi la Polisi linashirikisha wadau wa eneo husika pamoja na wadau wengine wa maeneo kwa maendeleo ili kufanikisha azma ya Serikali ya kujenga vituo vya kisasa vya polisi pamoja na nyumba za kuishi askari.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilayani Chemba Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, wananchi na wadau wengine wapo kwenye hatua za awali za kuanza ujenzi wa kituo cha polisi. Aidha, kwa sasa mchoro wa ramani ya kituo na gharama za ujenzi (BOQ) zimeshakamilika na ukusanyaji wa mahitaji ya ujenzi unaendelea.
Mheshimiwa Naibu Spika, naamini jitihada hizi zitaungwa mkono na Mheshimiwa Mbunge ili kuhakikishia wananchi wake usalama wao pamoja na mali zao.