Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 63 2018-04-12

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. JOSEPH R. SELASINI (K.n.y RHODA E. KUNCHELA) aliuliza:-
Kuna mgogoro kati ya Manispaa na wafanyabiashara wanaomiliki vibanda katika masoko ya Buzogwe Soko Kuu na Mpanda Hoteli ambapo Manispaa inawaongezea kodi wafanyabiashara hao bila makubaliano ya pande zote mbili:-
Je, Serikali ina mpango gani wa haraka wa kumaliza mgogoro huo maana ni muda mrefu sasa na wafanyabiashara wamefunga vibanda vyao wakisubiri muafaka na hivyo Serikali kushindwa kukusanya kodi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rhoda Edward Kunchela, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Halmashari ya Manispaa ya Mpanda imejenga vibanda vya biashara katika masoko kwa ubia baina ya Halmashauri na wafanyabiashara (wamiliki/ wajenzi). Masoko ambayo yaliongezewa ushuru wa pango ni masoko yanayomilikiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda ambayo ni soko kuu la Buzogwe na Azimio.
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda iliamua kufanya mabadiliko ya ushuru baada ya kubaini kuwa wamiliki/wajenzi walikuwa wakinijufaisha wenyewe kwa kuwapangisha wafanyabiashara na kuwatoza kodi kati ya Sh.100,000 hadi Sh.150,000 na kuwasilisha kodi ya Sh.15,000 tu kwa mwezi kwa Halmashauri.
Mheshimiwa Spika, mabadiliko ya kodi yaliyofanyika kwa wamiliki/wajenzi ni kutoka Sh.15,000 hadi Sh.40,000 kwa mwezi. Wadau wote walishirikishwa na makubaliano yaliridhiwa katika vikao vya kisheria vya Halmashauri. Aidha, hakuna maduka yaliyofungwa, huduma zinaendelea kama kawaida na Halmashauri imeendelea kukusanya mapato.
Mheshimiwa Spika, Halmashauri zinaweza kufanya marekebisho ya kodi wakati wowote. Utaratibu unaotumika katika kuibua na kuongeza kodi/tozo huanzishwa, huchakatwa na kuamuliwa na kikao cha Kamati ya Fedha, Uchumi na Mipango ya Halmashauri husika.