Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 11 Information, Culture, Arts and Sports Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo 90 2018-04-17

Name

Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI (K.n.y. MHE. NURU A. BAFADHILI) aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani madhubuti wa kuhakikisha vijana wetu wanakuwa na maadili pamoja na silka na desturi za Kitanzania kama walivyo wazazi wao?

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nuru Awadhi Bafadhili, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, nianze kwa kusisitiza kuwa wazazi na familia kwa ujumla ndiyo walezi wa kwanza wenye jukumu la makuzi ya mtoto kuanzia hatua za awali. Wazazi hufuatiwa na vyombo vya elimu kuanzia elimu ya awali, msingi, sekondari hadi elimu ya juu. Jukumu la kusimamia malezi na makuzi ya watoto na vijana ni pamoja na kuelimisha kwa maneno na vitendo kuhusu utambuzi wa mambo mema na mambo mabaya, mambo yanayofaha na mambo yasiyofaha yanayostahili na yasiyostahili yakiwemo masuala ya mavazi, kauli, staha, mwenendo pamoja na muonekano kwa vijana.
Mheshimiwa Spika, hatua ya awali ya malezi ya makuzi ikishapita ndipo wajibu mkubwa wa Serikali unajitokeza katika ukuaji wa vijana kupitia sera, kanuni, sheria, taratibu pamoja na miongozo na kwa kutumia majukwaa mbalimbali ya elimu na nasaha kama vile semina, warsha, makongamano, mikutano, maonesho pamoja na matamasha.
Mheshimiwa Spika, changamoto kubwa inayolikabili Taifa letu leo ni athari ya utamaduni wa nje kwa maadili, mila na desturi zetu kupitia muingiliano mkubwa wa watu wa dunia kwa njia ya utalii, biashara na kadhalika, vilevile kupitia maendeleo ya kasi ya TEHAMA. Pamoja na juhudi za Serikali kudhibiti wimbi la utamadunisho hasi nchini kwa kutumia sheria, kanuni na vilevile kuboresha mitaala yetu toka shule ya msingi hadi elimu ya juu ili izingatie elimu ya uraia, utaifa, uzalendo, mchango wa wazazi na wananchi kwa ujumla katika kufanikisha jitihada za Serikali hauna mbadala. (Makofi)