Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 13 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 106 2018-04-19

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA aliuliza:-
Je, ni nini kauli ya Serikali katika kushughulikia tatizo la migogoro ya mipaka katika Kambi za JKT Nachingwea na Kikosi Namba 41 Majimaji na vijiji vinavyozunguka Kambi hizo?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Elias Masala, Mbunge wa Nachingwea, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Wizara yangu inatambua kuwepo kwa migogoro katika maeneo mbalimbali kati ya Kambi za Jeshi na vijiji jirani au maeneo yaliyotwaliwa na Jeshi kwa maslahi mapana ya nchi yetu.
Mheshimiwa Spika, Kambi ya 41 KJ (Majimaji) ilipimwa mwaka 2005, wananchi waliokuwepo wakati wa upimaji idadi yao walikuwa 61. Katika Kambi ya 843 KJ ya JKT iliyopo Nachingwea mwaka 2009 Halmashauri ya Wilaya ya Nachingwea ilichukua jukumu la kuainisha mipaka kati ya Kambi hiyo na Kijiji cha Mkukwe. Wananchi waliokuwa ndani ya Kambi wakati wa kubaini mipaka hiyo walikuwa ni kaya tisa.
Mheshimiwa Spika, mwaka huu wa fedha 2018/2019 Wizara yangu imetenga bajeti kwa ajili ya uthamini na kulipa fidia kwa wananchi wanaostahili. Baada ya uthamini, wananchi wenye stahiki ya malipo watalipwa fidia zao kwa mujibu wa sheria na kanuni za fidia za ardhi zilizopo.