Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 15 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 117 2018-04-23

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA B. MWAIFUNGA (k.n.y. MHE. TUNZA I. MALAPO) aliuliza:-
Je, ni eneo gani limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanda cha Kubangua Korosho katika Manispaa ya Mtwara Mikindani?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani imetenga maeneo kwa ajili ya viwanda vya kubangua korosho kwa ajii ya wajasiliamali wadogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka 2014/2015 mpaka mwaka 2016/2017 Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani ilipanga na kupima viwanja vyenye ukubwa wa ekari 239.13 katika eneo la Mtepwezi na Mtawanya kwa ajili ya ujenzi wa viwanda vya kubangua korosho na maghala. Katika viwanja hivi jumla ya ekari 28.41 imegawiwa kwa mfumo wa wakfu wa kuhudumia zao la korosho (CIDTF) na Chama cha Ushirika cha Mtwara na Masasi (MAMCU) kwa ujenzi wa viwanda vya korosho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri ina jumla ya ekari 210.72 ambazo zipo tayari kwa ajili ya waombaji mbalimbali walio tayari kujenga viwanda hasa vya kuchakata korosho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Halmashauri inaendelea na utengaji wa maeneo kwa ajili ya ujasiliamali wadogo wadogo kwa mwaka 2016/2017. Halmashauri imetenga eneo lenye ukubwa wa ekari 7.8 kwa ajili ya wajasiliamali. Maeneo hayo yapo eneo la Chikongola, Skoya, Ufukoni A, Ufukoni Stendi na eneo la SIDO.