Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 23 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 193 2018-05-07

Name

Juma Othman Hija

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbatu

Primary Question

MHE. JUMA OTHMAN HIJA aliuliza:-
Mradi wa kupeleka Umeme Vijijini (REA) ni mradi ambao unaendelea kwa kasi kubwa nchi nzima.
Je, Serikali inaweza kutuambia ni kwa kiasi gani umeme huu umesambazwa nchi nzima (coverage) tangu mradi huu ulipoanza?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Juma Othman Hija, Mbunge wa Tumbatu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini imekamilisha utekelezaji wa Mradi wa REA I ambapo utekelezaji wake ulijumuisha ujenzi wa miundombinu ya umeme wa msongo wa kilovoti 11/33 wenye urefu wa kilometa 1,700; umeme wa msongo wa kilovoti 0.4/0.23 wenye urefu wa kilometa 800 na ufungaji wa transfoma 386. Jumla ya vijiji 231 vilipatiwa umeme na jumla ya wateja 22,100 waliungan`ishiwa umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa Mradi wa REA II ulijumuisha ujenzi wa miundombinu ya umeme wa msongo wa kilovoti 11/33 wenye urefu wa kilometa 17,740; ujenzi wa umeme wa msongo wa kilovoti 0.4/0.23 wenye urefu wa kilometa 10,970; ufungaji wa transfoma 4,100 za ukubwa tofauti na kuvipatia umeme vijiji 2,500 na kuunganishia umeme kwa jumla ya wateja 178,641 ambao ni sawa na asilimia 71.46 ya matarajio ya wateja 250,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa azma ya Serikali ni kupeleka umeme katika vijiji vyote kufika mwaka 2020/2021, Serikali kupitia Wakala wa Umeme Vijijini (REA) mwezi Julai 2017 ilianza kutekeleza mradi wa REA III kupitia grid extension na Densification itayopeleka umeme maeneo ambayo yaliyorukwa katika utekelezaji wa REA I na II.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuunganisha umeme maeneo ya pembezoni mwa miji (Peri-urban, electrification program), kusambaza umeme katika vijiji vyote ikiwa ni pamoja vilivyo pembezoni mwa mkuza wa njia ya msongo wa kilovoti 400 kutoka Iringa hadi Shinyanga na utekelezaji wa miradi ya nishati jadidifu. Utekelezaji wa miradi ya REA III kwa mzunguko wa kwanza unajumuisha ufunguji wa miundombinu ya umeme ya msongo wa kilovoti 11/ 33 yenye urefu wa kilometa 16,420; njia za umeme wa msongo wa kilo vote 0.4 lenye urefu wa kilometa 15,600; ufungaji wa transforma 6,700 na kuvipatia umeme vijiji zaidi 3,559 na kuwaunganisha wateja 300,000.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi mwezi Machi utekelezaji wa miradi mbalimbali ya umeme vijijini nchini umechangia kufikia matumizi jumla ya umeme nchini (overall access) kufikia asilimia 67.5 kwa vijijini ambapo vijijini ni asilimia 49.5 kutoka asilimia mbili iliyokuwepo wakati wakala unaanza kutekeleza majukumu yake mwaka 2007 na mijini ni asilimia 97.3.