Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 25 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 208 2018-05-09

Name

Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RISALA S. KABONGO aliuliza:-
Hospitali ya Wilaya ya Vwawa ambayo inatoa huduma kwa Halmashauri nne za Mbozi, Ileje, Songwe na Momba inakabiliwa na upungufu wa vifaatiba, wodi, watumishi pamoja na Madaktari Bingwa.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kupandisha hadhi Hospitali ya Vwawa kuwa Hospitali ya Mkoa ili iweze kutengewa bajeti ya kutosha kukabiliana na changamoto zilizopo sasa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Risala Said Kabongo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ilituma timu ya wataalam kutoka Idara mbalimbali na Hospitali ya Taifa Muhimbili ambayo ilifanya ukaguzi wa siku kumi kuanzia tarehe 25 Agosti, 2017 hadi 5 Septemba, 2017 katika Hospitali ya Vwawa iliyopo Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe ili kufanya tathmini kuona kama hospitali hiyo inaweza kutumika kama Hospitali ya Mkoa na hatimaye kuwasilisha matokeo ya tathmini hiyo kwa Mheshimiwa Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri aliridhia Hospitali ya Wilaya ya Mbozi yaani Vwawa itumike kwa muda kama Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe wakati Mkoa unaendelea na taratibu za kujenga Hospitali ya Mkoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuboresha huduma katika hospitali hii, Serikali ilipeleka watumishi tisa akiwemo Daktari Bingwa wa Magonjwa ya akina mama pamoja na kufunguliwa akaunti Bohari ya Dawa (MSD) yenye namba MB 310004 yenye kutoa mgao wa dawa ngazi ya mkoa ili kuweza kutoa huduma kama Hospitali ya Rufaa ya Mkoa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeshatoa kiasi cha shilingi milioni 767 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Songwe ambapo eneo lenye ukubwa wa hekari 23 lililopo Hasamba katika Mji Mdogo wa Vwawa limeshatengwa na taratibu za kuanza ujenzi wa Hospitali hiyo kwa awamu ya kwanza zimeshaanza ikiwemo uandaaji wa michoro ya usanifu inayofanywa na Wakala wa Majengo Tanzania. Inatarajiwa Wakala wa Majengo ndiye atasimamia ujenzi wa hospitali hiyo. (Makofi)