Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 25 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 214 2018-05-09

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi Wilaya ya Mlele?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua uhitaji wa vituo vya polisi pamoja na nyumba za kuishi askari kote nchini ikiwemo Wilaya ya Mlele. Ili kutatua changamoto hii, Serikali kupitia Jeshi la Polisi inashirikisha wananchi pamoja na wadau mbalimbali wengine wa maendeleo ili kufanikisha azma ya Serikali ya kujenga vituo vya polisi vya kisasa nchi nzima.
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na ufinyu wa bajeti na uhitaji wa vituo vya polisi katika maeneo mbalimbali nchini kuwa mkubwa, namwomba Mheshimiwa Mbunge kushiriki katika jitihada hizi kwa kuhamasisha wananchi wake kushiriki katika mpango huu ili kuhakikisha huduma za Kipolisi zinaimarika karika eneo hilo. (Makofi)