Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 27 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 229 2018-05-11

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:-
Je, ni lini Vijiji vya Jeje, Kashangu, Idodyandole, Mbugani, Aghondi, Mabondeni, Kitopeni, Ipande, Muhanga, Damwelu, Kitaraba, Kazikazi, Kintanula na Rungwa vitapatiwa umeme katika Mradi wa REA?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kupeleka umeme katika vijiji vyote vya Tanzania Bara ambavyo havijafikiwa na miundombinu ya umeme ili vifikiwe na umeme ifikapo mwezi Juni, 2021.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Jimbo la Manyoni Magharibi lina vijiji vipatavyo 39 ambapo vijiji 11 vimefikishiwa miundombinu ya umeme. Vijiji 10 vya Kamenyanga, Kayui, Jeje, Songa Mbele, Njirii, Kashangu, Idodyandole, Sanjaranda, Ziginali na Ipanga vimewekwa katika mradi wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza. Utekelezaji wa mradi huu umekwishaanza na mkandarasi anayefanya kazi hii katika Mkoa wa Singida aitwaye CCCE-ETERN Consortium anatarajia kukamilisha kazi Juni, 2019. Kazi za ujenzi zinajumuisha ujenzi wa kilometa 22.4 za njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 na kilometa 36 za njia za umeme wa msongo kilovoti 0.4/0.23, ufungaji wa transfoma 18 na uunganishwaji wa wateja 662. Gharama ya mradi huu ni shilingi bilioni mbili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji 18 vilivyobaki vikiwemo vya Mbugani, Aghondi, Maondeni, Kitopeni, Ipande, Muhanga, Damwelu, Kitaraba, Kazikazi, Kitamula na Rungwa vitaanza kupelekewa umeme kupitia mradi huu mzunguko wa pili kuanzia Julai, 2019 na kukamilika Juni, 2021.