Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 29 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 243 2018-05-15

Name

Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AMINA S. MOLLEL aliuliza:-
Je, ni kwa kiwango gani Serikali imetekeleza agizo la Bunge la kukusanya kodi katika huduma za mahoteli kwenye Hifadhi za Taifa kwa njia ya Concession Fee Fixed Rate?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Amina Saleh Mollel, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukusanyaji wa Tozo ya Concession Fees kwa utaratibu mpya wa Fixed Rate ulianza kutekelezwa tarehe 1 Julai, 2017 kwa mujibu wa Tangazo la Serikali Na.234 la mwaka 2017. Kwa mujibu wa Tangazo hilo, kila mgeni anatozwa kati ya Dola za Kimarekani 25 na 50 kulingana na hadhi ya hifadhi husika. Kwa mfano, Hifadhi ya Taifa ya Mikumi ni Dola za Kimarekani 25 na Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ni Dola 50 za Kimarekani. Kwa hivi sasa wawekezaji wote wanalipa tozo hiyo kwa viwango vilivyoainishwa katika Tangazo hilo la Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kiasi cha Tozo ya Concession Fees kilichokusanywa katika kipindi cha Julai, 2017 hadi Machi, 2020 kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ni shilingi bilioni
18.8 ikilinganishwa na shilingi bilioni 6.9 iliyokusanywa katika kipindi hicho mwaka 2016/2017. Hili ni ongezeko la shilingi bilioni 11.9 ambazo ni sawa na 174%.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyokusanywa kutoka katika makusanyo ya Tozo ya Concession Fees kwa kipindi hicho ni shilingi bilioni 3.4 ikilinganishwa na kipindi kama hicho cha mwaka wa fedha 2016/2017 ambapo jumla ya shilingi bilioni 1.2 zilikusanywa na kupelekwa TRA.