Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 29 Energy and Minerals Wizara ya Madini 244 2018-05-15

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itawapatia wachimbaji wadogo wadogo maeneo yaliyopimwa na kuwa na uwepo wa madini kama dhahabu, ikiwemo Moroko katika Mkoa wa Geita na maeneo mengine yenye madini nchini?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTO M. BITEKO) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Upendo Furaha Peneza, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu mwaka 1996, Serikali kupitia Wizara ya Madini imekuwa ikitenga maeneo maalum kwa ajili ya wachimbaji wadogo wa madini. Tangu kipindi hicho hadi sasa, Wizara ya Madini imetenga jumla ya maeneo 46 katika sehemu mbalimbali nchini yenye ukubwa wa hekta 281,533.69. Serikali kupitia Wizara ya Madini itaendelea kutenga maeneo kwa ajili ya wachimbaji wadogo kadiri yatakavyokuwa yanapatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wa Geita Wizara imetenga maeneo kwa ajili ya wachimbaji wadogo wa madini na kutoa leseni kama ifuatavyo: Eneo la Nyarugusu leseni 41; eneo la Rwamgasa leseni 36; eneo la Isamilo/ Lwenge leseni 22 na eneo la Mgusu leseni 22. Kwa sasa eneo la Moroko alilolitaja Mheshimiwa Mbunge lipo ndani ya leseni ya utafiti yenye Na.8278 ya mwaka 2012 inayomilikiwa na Mgodi wa Dhahabu wa Geita. Maeneo mengine ya mkoa huo yataendelea kutengwa kama ilivyoainishwa katika Kifungu cha 16 cha Sheria ya Madini ya mwaka 2010 na Marekebisho yake ya mwaka 2017.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Wizara kwa kutumia taasisi zake za GST pamoja na STAMICO itaendelea kufanya utafiti ili kubaini uwezo wa mashapo ya madini katika maeneo mbalimbali nchini na kuyatenga kwa ajili ya uchimbaji mdogo wa madini. Hii itawezesha wachimbaji wadogo wa madini kufanya kazi na kuchimba kwa uchimbaji wa tija. Ahsante.