Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 30 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 259 2018-05-16

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ISSA A. MANGUNGU aliuliza:-
(i) Je, ni lini ujenzi wa kituo kidogo cha kupoza umeme (substation) ya Mbagala utakamilika?
(ii) Je, makubaliano ya mkataba wa ujenzi wa kituo hicho ulikuwa wa muda gani?
(iii) Je, mkandarasi wa mradi huo yupo ndani ya muda au amechelewesha kazi kwa mujibu wa mkataba na je ni hatua gani zimechukuliwa?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ali Mangungu, Mbunge wa Mbagala, lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-
• Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme katika Jiji la Dar es Salaam hasa maeneo ya Mbagala, Shirika la Umeme nchini (TANESCO) mwezi Februari, 2018 kupitia Mradi wa TEDAP (Tanzania Energy Development and Access Expansion Project) lilikamilisha utekelezaji wa mradi wa uboreshaji wa njia za usafirishaji, usambazaji na vituo vya kupoza umeme katika Mikoa ya Dar es Salaam, Arusha na Kilimanjaro. Mradi huu ulitekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Dunia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kukamilika kwa mradi huu kumeimarisha upatikanaji wa umeme katika eneo la Mbagala ikilinganishwa na kipindi cha nyuma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme cha Mbagala ulikamilika na kuanza kufanya kazi rasmi kuanzia tarehe 25 Februari, 2018.
• Makubaliano ya awali ya mkataba wa ujenzi wa mradi mzima ikiwemo ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme cha Mbagala ulikuwa wa miezi 18 kutoka siku mkandarasi alipokabidhiwa maeneo ya ujenzi wa mradi.
• Mheshimiwa Mwenyekiti, mkandarasi amekamilisha kazi hii nje ya mkataba wa awali kutokana na kuzuiwa kufanya kazi katika baadhi ya maeneo kutokana na baadhi ya wananchi kudai kwamba hawakuridhika na fidia na hivyo kumfanya mkandarasi asikamilishe utekelezaji wa mkataba huu kwa wakati. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa hali ya umeme imeimarika katika maeneo ya Mbagala na Wizara yangu itaendelea kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi kuhakikisha hali ya umeme Mbagala inaendelea kuwa ya uhakika. Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.