Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 31 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 262 2018-05-17

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question


MHE. VEDASTO E. NGOMBALE aliuliza:-
Moja ya majukumu makubwa ya Serikali ni kulinda raia na mali zao kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama ikiwemo Polisi:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kukirejesha Kituo cha Polisi katika Tarafa ya Kipatimu Wilayani Kilwa ambacho kilihamishwa?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Vedasto Edgar Ngombale, Mbunge wa Kilwa Kaskazini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuwa Kituo cha Polisi cha Kipatimu kilifungwa mwaka 1998 kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo uchakavu wa miundombinu na mahusiano mabaya kati ya raia na Askari kiasi cha kutishia usalama wa Askari na mali za Serikali zilizoko kituoni.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa wananchi wameona umuhimu wa kurejesha huduma za Polisi katika eneo husika ambapo wameanza ujenzi wa kituo kipya cha Polisi. Aidha, nimshauri Mheshimiwa Mbunge kuwasiliana na Jeshi la Polisi Mkoa wa Lindi ili kuona namna bora ya kukamilisha ujenzi wa kituo hicho.