Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 33 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 279 2018-05-21

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. NURU A. BAFADHILI (K.n.y. MHE. REHEMA J. MIGILLA) aliuliza:-
Je, kwa nini Serikali haitaki kujenga Hospitali ya Wilaya ya Tabora Mjini baada ya Hospitali ya Wilaya kupewa hadhi ya Hospitali ya Rufaa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Rehema Juma Migilla, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mhemishimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali Na. 96 la tarehe 18/4/2018 lilioulizwa na Mheshimiwa Munde Tambwe Abdallah, Mbunge wa Viti Maalum, Serikali imeanza ujenzi wa Hospitali ya Wilaya Tabora Mjini tangu tarehe 19 Oktoba, 2015 kwa kuanza na jengo la OPD kwa gharama ya shilingi milioni 150 chini ya Mkandarasi HERU Construction Company Limited ambapo hadi sasa sehemu ya msingi, nguzo, ngazi na slabu vimekamilika kwa asilimia 100. Mkandarasi ameshalipwa jumla ya shilingi milioni 145.7 kutokana na fedha za ruzuku ya miradi ya maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2018/2019, Manispaa ya Tabora imetenga shilingi milioni 70 kwa ajili ya kuendelea na ujenzi wa jengo la OPD katika hospitali hiyo. Mkakati wa Serikali ni kuimarisha Vituo vya Afya 513 nchi nzima ili viweze kutoa huduma za dharura pamoja na kujenga Hospitali za Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati kwa kuweka kipaumbele kwenye maeneo yenye uhitaji mkubwa, ndiyo maana Serikali imepeleka jumla ya shilingi bilioni 2.6 Mkoa wa Tabora, kwa ajili ya ukarabati wa vituo sita vya Afya katika Wilaya za Nzega, Tabora-Uyui, Igunga, Kaliua na Urambo kupitia awamu ya kwanza na ya pili ya miradi ya afya iliyoanza kutekelezwa Septemba, 2017. Katika mwaka wa fedha 2018/2019, Serikali imetenga shilingi bilioni 101 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali za Wilaya 67 nchi nzima ambapo mbili kati ya hizo zipo katika Wilaya ya Uyui na Sikonge, Mkoani Tabora.