Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 34 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 287 2018-05-22

Name

Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. ALBERT O. NTABALIBA aliuliza:-
Akina mama na vijana wa Jimbo la Buhigwe wanajituma sana katika kilimo na uwekezaji.
(a) Je, ni lini Serikali itawasaidia kimtaji ili waweze kujikomboa?
(b) Je, ni kiasi gani kimetolewa kuwawezesha akina mama na vijana katika miaka ya 2010 hadi 2017?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Albert Obama Ntabaliba, Mbunge wa Buhigwe, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza viongozi wa Mkoa wa Kigoma kwa kuwahamasisha vijana wa Mkoa wa Kigoma kuanzisha vikundi vingi vya wajasiriamali ambavyo ni nyenzo muhimu katika kuleta maendeleo ya wanawake, vijana na wananchi kwa ujumla.
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuwasaidia wanawake na vijana kwa kuwapatia mikopo yenye masharti nafuu kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake na Vijana. Mikopo hii imelenga kuwasaidia kupata mitaji ya kuendeleza shughuli zao za kiuchumi hivyo kujiongezea kipato na kukuza uchumi.
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe imeanza kufanya kazi Januari, 2013 hivyo taarifa zilizopo ni kuanzia mwaka huo. Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2013/2014 hadi 2016/2017 Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe ilitoa jumla ya shilingi 25,377,057 kwa ajili ya kuvikopesha vikundi vya wanawake na vijana. Kwa mwaka wa fedha 2017/2018 hadi kufikia Mei, 2018 jumla ya shilingi 10,500,000 zimetolewa katika vikundi vya wanawake na vijana. Aidha, kupitia Mfuko wa Jimbo Mheshimiwa Mbunge alitoa shilingi 10,500,000 kwa vikundi saba vya bodaboda na kikundi kimoja cha mafundi seremala.
Mheshimiwa Spika, jumla ya shilingi 20,200,000 zimetengwa kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kwa ajili ya vikundi vya wanawake na vijana.