Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 39 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 321 2018-05-29

Name

Hassan Selemani Kaunje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE (K.n.y HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:-
Kuna mgogoro wa ardhi wa muda mrefu kati ya wananchi wa kijiji cha Mkwaya na mwekezaji Durbali:-
Je, ni lini mgogoro huo utapatiwa ufumbuzi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Selemani Kaunje, Mbunge wa Lindi Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna mgogoro unaowahusisha baadhi ya wananchi wa Manispaa ya Lindi ambao wako kwenye Mitaa ya sokoni, Makonde na Mtere ambayo zamani ilikuwa ni sehemu ya Kijiji cha Mkwaya ambao wanasemekana kuvamia na kugawana mashamba yanayomilikuwa na Kampuni ya Indo-African Estate Limited.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mgogoro huu si kati ya wananchi hao na bwana Amin Durbali ambaye ni mmoja kati ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Indo-African Estate Limited bali ni kati ya wananchi na Kampuni ya Indo-Africa Estate Limited ambayo ndiyo ina hatimiliki za mashamba hayo yenye ukubwa wa ekari 3,601.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kampuni ya Indo-African Estate Limited ilifungua Kesi Na.17 ya mwaka 2015, ambayo hukumu yake imetolewa Februari, 2018 na kuipa Serikali ushindi. Kinachoendelea sasa ni taratibu za kufuta miliki za mashamba hayo kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi Na.4 ya mwaka 1999 na Kanuni zake za mwaka 2001. Baada ya kufutwa kwa miliki za mashamba hayo, Serikali itaweka utaratibu mzuri wa ugawanaji wa mashamba hayo kwa wananchi.