Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 39 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 325 2018-05-29

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:-
Tatizo la wahamiaji haramu hasa kutoka Ethiopia limeshamiri sana katika nchi yetu kwa sasa:-
(a) Je, ni wahamiaji haramu wangapi wamekamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria?
(b) Kama wapo ambao wanaendelea na kifungo, je, ni hatua gani za kisheria ambazo zinachukuliwa baada ya kutolewa kifungoni?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Fakharia Shomar Khamis, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) yote kwa pamoja, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Idara ya Uhamiaji imekamata jumla ya wahamiaji haramu 13,393 katika kipindi cha Julai, 2017 hadi Machi 2018. Miongoni mwao wahamiaji haramu 2,815 walishtakiwa, 117 walitozwa faini, 429 walifungwa, 6,316 waliondoshwa nchini, 1,353 waliachiwa huru baada ya kutoa nyaraka za uthibitisho wa ukaazi wao. Aidha, zipo kesi 2,363 zinazoendelea katika mahakama mbalimbali nchini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua za kisheria ambazo huchukuliwa baada ya wahamiaji haramu kumaliza vifungo vyao gerezani ni kurudishwa nchini kwao.