Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 58 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 490 2018-06-26

Name

Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. JAKU HASHIM AYOUB aliuliza:-
Mawaziri kama walivyo viongozi wengine wa Serikali, wapo kwa ajili ya kuwahudumia wananchi na kwamba wananchi wamewachagua Wabunge na Mawaziri (Serikali) ili kuwasiliana, kushirikiana na kushauriana katika kutatua kero zao; lakini kwa bahati mbaya sana wapo baadhi ya Mawaziri ambao kupatikana kwao hata kwenye simu ni jambo gumu kupita kiasi:-
a) Je, Serikali haioni kuwa ipo haja ya Mawaziri wenye tabia hiyo ya kujichimbia na kutopatikana kwenye simu kuacha tabia hiyo kwa maslahi ya wananchi?
b) Je, Serikali itakubaliana nami kuwa ipo haja ya kuweka utaratibu maalum wa kuifikia Serikali iwapo wananchi kupitia Mbunge wao wana shida ya kumuona Waziri anayehusika na akawa hapatikani hata kwa simu?

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS (MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jaku Hashim Ayoub, Mbunge anayewakilisha pia Baraza la Wawakilishi, lenye sehemu (a) na (b), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Kanuni B.3(1) ya Kanuni za Kudumu za Utumishi wa Umma za mwaka 2009, simu ni moja ya njia za mawasiliano halali Serikalini. Waheshimiwa Mawaziri wanafanya kazi zao kwa lengo la kuwahudumia wananchi na wananchi nao wana nafasi ya kutoa maoni na shida zao na hatimaye kupata mrejesho. Mpaka sasa Serikali haina ushahidi wa kuwepo Mawaziri ambao kwa makusudi hujichimbia na kutopatikana kwa simu. (Makofi)
(b) Mheshimiwa Spika, zipo njia mbalimbali ambazo wananchi wanaweza kuzitumia kuwasilisha maoni na kero zao ofisini kwa Waziri licha ya simu peke yake. Wananchi wanaweza kuandika barua, kupiga simu, barua pepe kwa viongozi na watendaji wa Wizara kama Makatibu Wakuu au Makatibu wa Waheshimiwa Mawaziri na taarifa za wananchi zitamfikia Mheshimiwa Waziri na kufanyiwa kazi.