Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 15 2018-09-05

Name

Jerome Dismas Bwanausi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA - (K.n.y. MHE. JEROME D. BWANAUSI) aliuliza:-
Madaraja ya Mwitika – Maparawe, Mipande – Mtengula na Mbangara – Mbuyuni yalisombwa na maji wakati wa mafuriko miaka mitano iliyopita na kusababisha matatizo makubwa ya usafiri:-
Je, ni lini Serikali itajenga madaraja hayo ili kuondoa adha ya usafiri inayowakabili wananchi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jerome Dismasi Bwanausi Mbunge wa Lulindi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba madaraja ya Mwitika, Maparawe, Mputeni, Mtengula na Mbangala, Mbuyuni yalisombwa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha mwaka 2015/2016. Kwa kutambua umuhimu wa barabara hii Serikali ilifanya tathmini juu ya gharama za ujenzi wa madaraja hayo, ilibainika kuwa kiasi cha shilingi bilioni 3.5 zinahitajika kukamilisha ujenzi wa madaraja hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kiasi hicho cha fedha ni kikubwa Serikali kupitia Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa imeweka kwenye maombi maalumu, hivyo ujenzi wake utategemea kuanza pindi fedha hiyo iliyoombwa itakapopatikana. Madaraja hayo yatahudumiwa na Wakala wa Huduma za Barabara Vijijini yaani TARURA.