Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 2 Energy and Minerals Wizara ya Madini 17 2018-09-05

Name

Ajali Rashid Akibar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MHE. AJALI R. AKBAR aliuliza:-
Madini aina ya Coltan yamegundulika katika Wilaya za Ruangwa, Masasi na Newala, lakini Wizara ya Madini imeweka beacon katika Kijiji cha Nandimba, Kata ya Chilagala.
(a) Je, ni utaratibu gani umetumika kuweka beacon katika Wilaya nyingine?
(b) Je, Serikali haioni kupora rasilimali ya wilaya nyingine kunaweza kusababisha migogoro?
(c) Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro huo?

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Madini, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rashid Akbar Ajali, Mbunge wa Jimbo la Newala Vijijini lenye sehemu (a), (b)na (c) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ya Ruangwa, Masasi na Newala hakuna uthibitisho wa uwepo wa madini aina ya Coltan yaliyogunduliwa. Madini yaliyogunduliwa katika Wilaya hizo ni aina ya Graphite yaani madini ya Kinywe ambapo baadhi ya Kampuni zimepewa leseni za utafiti na uchimbaji wa madini hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya mwaka 2010 na marekebisho yake ya mwaka 2017 na Kanuni zake, mmiliki wa leseni anatakiwa kuweka alama (beacon) zinazoonesha mipaka ya leseni yake ili jamii inayozunguka maeneo hayo ijue mwisho wa leseni husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, beacon zilizopo katika Kijiji cha Namlimba ziliwekwa na Kamuni ya Natural Resources Limited wakati wa ukusanyaji wa taarifa muhimu. Kampuni hii ya Natural Resources Limited ina umiliki wa leseni ya utafiti wa madini ya Graphite yenye nambari PL 10644/2015 ambayo mipaka yake inaingia kwenye Wilaya za Masasi na Newala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haina lengo la kupora rasilimali ya Wilaya nyingine bali lengo lake ni kuhakikisha kuwa rasilimali madini zinazopatikana katika eneo husika, zinanufaisha wananchi wake na taifa kwa ujumla. Hadi sasa kampuni hiyo inaendelea na shughuli za utafiti wa madini ya graphite (kinywe). Pindi itakapogundulika uwepo wa mashapo ya kutosha, taratibu za kuvuna rasilimali hiyo kwa manufaa ya Watanzania wakiwemo wananchi wa Wilaya ya Newala zitafanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi sasa Kampuni ya Natural Resources Limited haina mgogoro wowote na wananchi wa maeneo hayo. Namwomba Mheshimiwa Rashid Akbar Ajali kama kuna tatizo la mipaka ya kiutawala katika Wilaya za Masasi na Newala suala hilo liwasilishwe kwenye Wizara husika kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi.