Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 2 Justice and Constitutional Affairs Wizara ya Katiba na Sheria 25 2018-09-05

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKARI aliuliza:-
Kiswahili ndiyo lugha ya Taifa letu na kinapaswa kutumika katika nyanja zote ili kukipa hadhi yake:-
Je, kwa nini baadhi ya Mahakama nchini zinatumia lugha ya Kiingereza wakati zinapoendesha mijadala yake na katika kutoa hukumu?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (K.n.y. WAZIRI WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Katiba na Sheria, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Faida Bakari, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, matumizi ya lugha katika Mahakama zetu yamewekwa kwa mujibu wa sheria. Kwa mujibu wa kifungu cha 13(1) na (2) cha Sheria ya Mahakama za Mahakimu, Sura ya 11 (The Magistrates Courts Act, Cap 11) lugha inayotumika kuendesha kesi katika mahakama za mwanzo ni Kiswahili. Vile vile lugha itakayotumika katika mahakama ya Hakimu Mkazi na Mahakama ya Wilaya ni Kiswahili au Kiingereza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, shauri linaweza kuendeshwa kwa lugha yoyote kwa maelekezo ya Hakimu anayeendesha kesi katika Mahakama hizo, japokuwa kumbukumbu za shauri na maamuzi zinapaswa kuandikwa katika lugha ya kiingereza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hali kadhalika kwa mujibu wa Kanuni ya Pili ya Kanuni za Lugha za Mahakama na Kanuni ya Tano ya Kanuni za Mahakama ya Rufani ya Mwaka 2009, lugha itakayotumika kuendesha mashauri katika Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani ni Kiswahli au Kiingereza kutegemea na maelekezo ya Jaji au Mwenyekiti wa Jopo la Majaji japokuwa kumbukumbu na maamuzi ya shauri vinapaswa kuandikwa katika lugha ya Kiingereza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuendelea kutumika kwa Kiswahili katika Mahakama zetu na hukumu kuandikwa kwa Kiingereza kunatokana na kwamba Tanzania ni Mwanachama wa Jumuiya ya Madola na inafuata mfumo wa Common Law. Kwa kuandika hukumu kwa lugha ya Kiingereza imewezesha Mahakama za nchi nyingine za Jumuiya ya Madola kutumia hukumu zetu kama rejea na vivyo hivyo Tanzania kutumia hukumu za nchi nyingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kulihakikishia Bunge lako Tukufu kuwa sheria, kanuni na taratibu za uendeshaji wa mashauri katika Mahakama zetu unaruhusu kutumia lugha zote mbili, Kiswahili au Kiingereza na Mahakama zetu zimekuwa zikizingatia hilo.