Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 5 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 59 2018-09-10

Name

Issa Ali Abbas Mangungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. EDWIN A. NGONYANI (K.n.y. MHE. ISSA A. MANGUNGU) aliuliza:-
a) Je, Serikali ina mpango gani wa kusambaza umeme kwenye maeneo ambayo hayamo katika miradi ya umeme vijijini, maeneo kama vile Changanyikeni, Ponde, Malela, Vikindu, Goroka A, B katika Kata ya Tuangoma na Majimatitu A, Vigozi, Machinjioni A, Mponda katika Kata ya Mianzini, Mzala, Kwa Mapunda, Kisewe, Dovya, Sai A, B katika Kata ya Chamazi?
b) Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la low voltage katika Jimbo la Mbagala hasa maeneo ya Kiburugwa, Kilungule, Charambe, Kijichi, Kibondemaji Chemchem na Tuangoma?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ali Mangungu, Mbunge wa Mbagala, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kazi ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme katika maeneo ya Changanyikeni, Ponde, Malela, Vikindu, Goroka ‘A’ na Goroka ‘B’, Dovya Kata ya Tuangoma na maeneo ya Mponda, Vigozi, Churuvi Kata ya Mianzini ilianza Oktoba, 2017 na inatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba, 2018.
Mheshimiwa Spika, kazi za mradi zinahusiana ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 12.95, njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 41.34, pamoja na ufungaji wa transfoma 19 za Kv 100 na Kv 200, gharama ya mradi ni shilingi milioni 523.84 na utekelezaji wake umefikia asilimia 90.
Mheshimiwa Spika, Jimbo la Mbagala hususan maeneo ya Kiburugwa, Kitungule, Charambe, Kijichi, Kibondemaji, Chemchem na Tuangoma kulikuwa na tatizo la uwepo wa umeme mdogo, kuanzia mwezi Juni, 2018 Serikali imechukua hatua za makusudi kuondoa tatizo hilo kwa kuboresha nguvu ya umeme kwenye maeneo hayo na hali ya umeme katika maeneo ya Mbagala imeimarika kwa kiasi kikubwa.
Mheshimiwa Spika, kukamilika kwa ujenzi wa kituo kipya cha kupoza umeme cha msongo wa kilovoti 132/33 chenye uwezo wa Mv 50 Mbagala kilichozinduliwa tarehe 22 Februari, 2018 kimeimarisha hali ya umeme katika maeneo hayo. Ahsante. (Makofi)