Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 6 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 78 2018-09-11

Name

Mwantakaje Haji Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Bububu

Primary Question

MHE. MWANTAKAJE HAJI JUMA aliuliza:-
Zipo benki zinazotoa mikopo ya kilimo hususan Benki ya Kilimo Tanzania:-
Je, kwa upande wa Zanzibar ni wananchi wangapi wanaofaidika na mikopo ya kilimo?

Name

Dr. Ashatu Kachwamba Kijaji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kondoa

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti,kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwantakaje Haji Juma, Mbunge wa Bububu kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, jumla ya wananchi walionufaika na mikopo inayotolewa na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania kwa wananchi wa Zanzibar hadi kufikia tarehe 31 Julai, 2018 ni 3,000. Kati ya hao wanaume ni 1,800, wanawake 900 na vijana wa kike na kiume ni 300. Aidha, jumla ya mikopo iliyotolewa kwa idadi hiyo ya wananchi wa Zanzibar hadi kufikia tarehe 31Julai, 2018 ni shilingi bilioni 6.50.