Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 9 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 117 2018-09-14

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:-
Serikali imekuwa na mpango kabambe wa kupeleka umeme vijijini:-
Je, ni lini Serikali itawapelekea umeme wananchi wa Kata Itandula, Nyololo Shuleni, Maduma, Udumka, Kilolo, Kiyowole na Idete?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza kuanzia Julai, 2017 hadi Juni 2019. Katika Wilaya ya Mufindi jumla ya vijiji 53 vitapatiwa umeme kupitia mradi huu unaotekelezwa na mkandarasi Kampuni ya Sengerema Engineering Group Limited aliyepewa kazi za mradi huo kwa Mkoa wa Iringa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Mufindi Kusini, mradi utapeleka umeme katika Kata za Makungu, Igowole, Mninga, Nyololo, Isalavanu, Mbalamaziwa na Kasanga ambapo Vijiji vya Lugolofu, Mukungu, Lugema, Ibatu, Kisasa, Makalala, Ikwega, Itulituli, Lwing’ulo, Njojo, Nyololo Shuleni, Mjimwema, Idetero, Kimandwete, Ukemele, Udumuka, Lyang’a, Kilolo, Ihomasa pamoja na Maduma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi za mradi katika Wilaya ya Mufindi zinahusisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 139.63, njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 170, ufungaji wa transfoma 85 za kVA 50 na 100, pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 2,596. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 11.92. Kwa sasa mkandarasi ameshasimika nguzo za umeme wa line kubwa za HT kwa asilimia 90 na nguzo za umeme wa line ndogo LV kwa asilimia 95 kwa jimbo la Mufindi Kusini. Kazi ya ufungaji transfoma na kuunganisha wateja itaanza mwishoni mwa Septemba, 2018.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji vingine vya Kata ya Itandula, Kiyowole na Idete vitapatiwa umeme katika mzunguko wa pili wa mradi wa REA III unaotarajia kuanza Julai, 2019 na kukamilika Juni, 2021. Ahsante.