Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 12 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 121 2018-09-14

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. EZEKIEL M. MAIGE aliuliza:-
Jeshi la Polisi kupitia IGP Ernest Mangu ambaye alifanya ziara Wilayani Kahama mapema mwezi Agosti, 2016 alitangaza kuanzisha Mkoa mpya wa Kipolisi wa Kahama na Wilaya za Kipolisi za Msalala, Ushetu na Kahama; na wilaya hizo mpya za kipolisi zinakabiliwa na uhaba mkubwa wa askari na vitendea kazi vyao hasa vyombo vya usafiri:-
i. Je, ni watumishi wangapi wamepangwa Wilaya mpya ya Kipolisi ya Msalala?
ii. Je, Serikali iko tayari kusaidia vyombo vya usafiri hasa magari na pikipiki Wilaya ya Kipolisi ya Msalala?
iii. Je, Serikali imejipangaje kujenga ofisi za polisi wilaya na nyumba za makazi kwa askari katika Wilaya za Msalala, Ushetu na Kahama Mjini?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ezekiel Magolyo Maige, Mbunge wa Msalala, lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua uhitaji wa huduma ya kipolisi katika maeneo ya Ushetu, Msalala na Kahama. Aidha, maombi ya Msalala kuwa Wilaya ya Kipolisi yameshakamilika na maombi ya Kahama kuwa Mkoa wa Kipolisi yanaendelea kuzingatiwa. Kwa sasa Wilaya ya Msalala ina jumla ya maofisa, wakaguzi na askari wa vyeo mbalimbali 57.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni nia ya Serikali kuona kuwa vitendea kazi kwa Jeshi la Polisi vinapatikana ili kurahisisha utoaji wa huduma za polisi kwa wananchi. Wilaya mpya ya Msalala imepatiwa mgao wa gari moja jipya na taratibu za usajili zitakavyokamilika gari hilo litapelekwa Msalala kwa ajili ya kuhudumia wananchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ya Msalala, Ushetu na kahama Mjini ni miongoni mwa wilaya 65 nchini ambazo hazina majengo ya vituo vya polisi vyenye hadhi ya wilaya. Hata hivyo, halmashauri ya wilaya imeshatenga eneo kwa ajili ya ujenzi wa kituo na makazi ya askari na ujenzi utaanza mara pale fedha zitakapokuwa zimepatikana.