Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 47 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 396 2018-06-08

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY (K.n.y. MHE. DKT. MARY M. NAGU) aliuliza:-
Katika msimu wa mwaka 2015/2016, Wilaya ya Hanang ilikumbwa na mvua kubwa sana iliyosababisha kuharibika kwa miundombinu ikiwemo ya barabara.
(a) Je, ni kiasi gani cha fedha kilitengwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017 kwa ajili ya ukarabati wa barabara hizo?
(b) Je, ni lini Serikali itajenga na kukamilisha barabara iliyofunguliwa na Wachina inayopita katika Vijiji vya Mig’enyi, Milongoli, Gawidu hadi Ngamu na barabara inayounganisha Sechet, Wilaya ya Babati Vijijini kupitia Vijiji vya Basodesh, Basotu mpaka Mulbadaw?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Mary Michael Nagu, Mbunge wa Hanang lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara zilizoharibika ziliandaliwa maombi ya fedha za dharura ambapo barabara ya Getasam – Mto Bubu ilikarabatiwa kwa shilingi milioni
438.259 katika mwaka wa fedha 2015/2016. Barabara ya Basotu – Basodesh katika mwaka wa fedha 2016/2017 ilitengewa shilingi milioni 455 zilizotumika kujenga daraja moja lenye urefu wa mita 20 na kukarabati barabara hiyo urefu wa kilometa sita kwa kiwango cha changarawe.
(b) Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi Februari, 2018 Mfuko wa Barabara ulitoa fedha za dharura shilingi milioni 500 kwa ajili ya matengenezo ya barabara ya Ming’enyi – Milongori. Katika bajeti ya mwaka wa fedha 2018/2019, barabara za Endasak – Gitting – Dawar – Gawal – Gawidu zimeombewa shilingi milioni 209 za kuzifanyia matengenezo. Aidha, barabara ya Basotu – Basodesh imeombewa shilingi milioni 90 za kuwezesha ujenzi wa daraja linalounganisha Wilaya ya Hanang na Babati Vijijini.