Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 43 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 361 2018-06-04

Name

John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU aliuliza:-
Kabla ya kuanzishwa Shule za Kata, kulikuwa na mpango wa kujenga shule katika tarafa. Kwenye Jimbo la Ulyankulu kulijengwa shule tatu ambazo ni Kashishi, Ulyankulu na Mkindo; Shule ya Kashishi hivi sasa ina kidato cha tano na sita:-
Je, ni lini Shule za Mkindo na Ulyankulu zitapewa hadhi ya kuwa na kidato cha tano na sita ili kuwapunguzia wanafunzi gharama za kufuata mbali masomo ya kidato cha tano na sita?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa John Peter Kadutu, Mbunge wa Ulyankulu, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa, naomba kwa ruhusa yako niondoe sentensi moja tu inayoanza na neno Tarafa mpaka pale mwisho na sita.
Mheshimiwa Spika, malengo ya Serikali kwa sasa ni kuhakikisha kuwa, kila Tarafa angalau ina shule moja yenye kidato cha tano na sita. Mkakati uliopo kwenye maeneo ambayo tayari kuna shule zinazotoa elimu ya kidato cha tano na sita ni kuziimarisha kwa kuziwekea miundombinu, kuzipatia vifaa vya kufundishia na kujifunzia na kuzipatia Walimu wa kutosha.
Mheshimiwa Spika, ili shule iweze kupandishwa hadhi na hatimaye kusajiliwa kama Shule ya Kidato cha Tano na Sita ni lazima itimize vigezo vifuatavyo:-
(a) Iwe na miundombinu inayojitosheleza kama mabweni, madarasa, bwalo, jiko na maktaba;
(b) Iwe na huduma muhimu na za uhakika za maji na umeme; na
(c) Iwe na Walimu wa kutosha.
Mheshimiwa Spika, kwa muktadha huo, Shule za Sekondari Ulyankulu na Mkindo bado zina changamoto ya miundombinu isiyojitosheleza kama mabweni, madarasa, bwalo, jiko na maktaba. Hivyo, naishauri Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua ifanye jitihada za makusudi kuwezesha shule hizo mbili kufikia vigezo vinavyohitajika ili ziweze kusajiliwa. Aidha, kwa kuwa bajeti ya Wizara ya Elimu pamoja na ile Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa mwaka 2018/2019 zimeshapitishwa na Bunge, itakuwa vigumu shule hizo kusajiliwa na kuanza kuchukua wanafunzi wa mwaka huo.