Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 53 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 452 2018-06-19

Name

Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI aliuliza:-
Wananchi wa Kagera wana tatizo la umeme na umeme wa REA II umeingia katika center za vijiji tu.
Je, ni lini wananchi hao watapatiwa umeme ili waondokane na adha ya kutumia vibatari?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Alfredina Aporinary Kahigi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, awamu ya pili ya utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini ililenga pamoja na mambo mengine kufikisha umeme katika maeneo ya njia kuu, baadhi ya maeneo muhimu katika vijiji na katika taasisi za umma. Utekelezaji wa miradi ya REA Awamu ya Pili ulikamilika mwezi Desemba, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ilianza kutekeleza Mradi wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza tangu mwezi Julai, 2017. Katika Mkoa wa Kagera vijiji vipatavyo 141 vinatarajia kupatiwa umeme kupitia mradi huu. Mradi huu utakamilika mwezi Juni, 2019. Kazi ya kupeleka umeme katika vijiji hivi inahusisha ujenzi wa njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilometa 299, njia ya umeme wa msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilometa 574, ufungaji wa transfoma 287 za KVA 50 na 100 pamoja na kuunganishia umeme wateja wa awali 9,136. Gharama za mradi ni shilingi bilioni 38.
Mheshimiwa Naibu Spika, hadi kufikia mwezi Aprili, 2018 mkandarasi Kampuni ya Nakuroi Investment Ltd. aliyepewa kazi ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme katika Wilaya zote za Mkoa wa Kagera alikuwa ameshakamilisha kazi ya upimaji wa maeneo yatakayopelekewa umeme. Kazi zinazofanyika sasa ni kusambaza nguzo katika maeneo ya mradi na kujenga miundombinu, pamoja na kusambaza umeme.