Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 54 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 457 2018-06-20

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA aliuliza:-
Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Nyamagana linalojengwa katika Kata ya Mkolani limechukua zaidi ya
miaka minne sasa bila kukamilika:-
(a) Je, Serikali haioni kuwa na miradi isiyokamilika kwa wakati kunarudisha nyuma maendeleo;
(b) Je, ni lini sasa Serikali itapeleka fedha za kukamilsha jengo hilo?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stanslaus Shing’oma Mabula, Mbunge wa Nyamagana, lenye vipengele (a) na (b), kwa pamoja kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba ujenzi wa jengo la Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana ulioanza mwaka wa fedha 2008/2009 umechukua muda mrefu. Sababu kubwa ya kuchelewa kukamilika kwa ujenzi huo ni changamoto ya upatikanaji wa fedha za ruzuku ya maendeleo. Hadi sasa kiasi cha shilingi bilioni 1.34 kati ya shilingi bilioni 1.84 zilizokuwa zinahitajika zimetolewa na kutumika katika kujenga boma lenye vyumba 23 vya ofisi, kumbi mbili, mgahawa, chumba cha kuhifadhia nyaraka, vyoo, kuezeka jengo lote, kupiga plasta, kuweka milango, vigae, kupaka rangi, kuweka dari, kufunga milango na madirisha na mfumo wa maji safi na maji taka.
Mheshimiwa Spika, kwa kutambua umuhimu wa kumaliza jengo hilo, jumla ya shilingi milioni 420 zimetengwa katika mwaka wa fedha 2018/2019 ili kumalizia mfumo wa usalama wa jengo ikiwemo zimamoto, mfumo wa umeme, tanki la maji na uzio. Kwa maana hiyo, ujenzi wa jengo hilo unatarajiwa kukamilika katika mwaka wa fedha 2018/2019.