Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 54 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 464 2018-06-20

Name

Devotha Methew Minja

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEVOTHA M. MINJA aliuliza:-
Serikali iliahidi kutaifisha mashamba makubwa ya uwekezaji yasiyoendelezwa:-
Je, mpaka sasa mashamba mangapi yametaifishwa?

Name

William Vangimembe Lukuvi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ismani

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Devotha Mathew Minja, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Morogoro, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuchukua hatua dhidi ya wamiliki wote wa ardhi nchini ambao wameendelea kukiuka masharti ya umiliki yaliyomo katika Hati Miliki walizopewa. Kwa upande wa mashamba, Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli katika kipindi cha kuanzia mwaka 2015, Disemba mpaka sasa imebatilisha miliki za mashamba 32 yenye ukubwa wa jumla ya ekari 67,393.6, Mashamba haya yapo katika Halmashauri za Kinondoni, Temeke, Kilosa, Mvomero, Morogoro, Iringa, Kibaha, Busega, Muheza, Lushoto, Bukoba na Arumeru.
Mheshimiwa Spika, mbali na mashamba hayo Wizara yangu imeendelea kupokea mapendekezo ya kubatilisha miliki za mashamba yasiyoendelezwa kutoka kwenye Halmashauri mbalimbali nchini, zikiwemo Halmashauri za Wilaya ya Tarime, Serengeti na Mkinga ambapo taratibu za ubatilishaji wa mashamba hayo zinaendelea kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Spika, natoa wito kwa Halmashauri zote nchini ambazo zimebaini kuwepo kwa mashamba yasiyoendelezwa au mashambapori katika maeneo yao kuendelea kuwahimiza Maafisa Ardhi wa Wilaya zao kutuma ilani za ubatilisho au ilani za utelekezaji ardhi kwa wamiliki wa mashamba hayo kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi, Sura 113 na kuwasilisha mapendekezo ya kubatilisha miliki za mashamba hayo katika Wizara yangu ili taratibu za kuyabatilisha zikamilishwe kwa mujibu wa sheria.