Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 57 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 485 2018-06-25

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. SEIF K.S. GULAMALI aliuliza:-
Je, ni lini utekelezaji wa usambazaji wa umeme katika Kata za Igoweko, Uswaya, Tambarale, Mwisi, Sungwizi, Mwamala, Ntobo, Ngulu, Mwashiku na Kitangiri utaanza?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Seif Khamis Gulamali, Mbunge wa Manonga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, utekelezaji wa usambazaji wa umeme katika Kata za Igoweko, Uswaya, Tambarale, Mwisi, Sungwizi, Mwamala, Ntobo, Ngulu, Mwashiku na Kitangiri utafanyika kupitia mradi wa REA Awamu ya Tatu mzunguko wa kwanza wa kusambaza umeme vijijini iliyoanza mwezi Julai, 2017 na kukamilika Juni, 2019.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya kusambaza umeme katika kata hizi inajumuisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 zenye urefu wa kilomita 76.48; njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 60.62; ufungaji wa transfoma 36 za KVA 50 pamoja na kuunganisha wateja wa awali 733. Gharama ya kazi hii ni shilingi bilioni 1.22. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.