Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 22 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 177 2018-05-04

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. DKT. DAVID M. DAVID) aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itapeleka waganga, watumishi wa afya pamoja na vitendea kazi katika zahanati za Same Magharibi zilizojengwa kwa ushirikiano wa wananchi?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt.David Mathayo, Mbunge wa Same Magharibi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatambua tatizo la upungufu wa watumishi wa sekta ya afya katika Jimbo la Same Magharibi, ambapo mahitaji ni watumishi 867 lakini waliopo ni 287, upungufu ni watumishi 585.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2017/2018, Serikali imepeleka watumishi wapya 10 wa sekta ya afya katika jimbo hilo. Katika mwaka wa fedha 2018/2019, Halmashauri ya Wilaya ya Same imeomba kibali cha kuajiri watumishi wapya 104 wa sekta ya afya ambao watapangwa katika vituo vyenye upungufu mkubwa wa watumishi.