Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 24 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 198 2018-05-08

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. ALEX R. GASHAZA aliuliza:-
Kwa muda mrefu kumekuwepo na tatizo kubwa la hali ya usalama katika Jimbo la Ngara tangu mwaka 1993 kutokana na kuwa mpakani mwa nchi za Rwanda na Burundi ambapo kuna mwingiliano mkubwa wa wageni/wahamiaji haramu kutoka nchi hizo.
(a) Je, ni lini Serikali itaanzisha Kanda Maalum ya Kipolisi katika Wilaya ya Ngara ili kudhibiti hali ya usalama?
(b) Je, ni lini Serikali itajenga vituo vya polisi katika Kata ya Mabawe, Muganza, Kirushya, Mtobeye, Mbuba na Nyakisasa?
(c) Kwa kuwa Jeshi la Polisi Wilayani Ngara lina gari moja tu zima na lingine bovu bovu, je, ni lini Serikali itatupatia angalau magari mawili, moja kwa ajili ya Tarafa ya Rulenge na la pili kwa ajili ya Tarafa ya Murusagamba?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Alex Gashaza, Mbunge wa Ngara lenye sehemu (a), (b) na (c) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, hali ya usalama katika Jimbo la Ngara kwa sasa imeimarika ikilinganishwa na miaka iliyopita. Wilaya ya Ngara imepakana na nchi jirani za Rwanda na Burundi. Serikali imeweka mikataba ya ujirani mwema na nchi za Rwanda ambapo Jeshi la Polisi hufanya doria za pamoja mipakani.
Mheshimiwa Spika, kuna changamoto katika mipaka yetu na nchi ya Burundi inayotokana na kukosekana kwa amani katika nchi hiyo na kupelekea watu kuvuka mipaka. Aidha, Jeshi la Polisi nchini limeanzisha vituo vya ulinzi shirikishi ili kujenga uhusiano wa pamoja na wananchi ili kuimarisha hali ya usalama katika eneo hilo. Kwa sasa hali ya usalama katika eneo hilo imeimarika na hakuna haja ya Serikali kuanzisha Kanda Maalum ya Kipolisi.
Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua tatizo la uhaba wa vituo vya Polisi katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Wilaya ya Ngara na katika Kata za Mabawe, Muganza, Kirushya, Mtobeye, Mbuba na Nyakisasa. Aidha, katika Kata ya Muganza kitajengwa Kituo cha Polisi eneo la Mkalinzi kwa nguvu za wananchi ambapo katika Kata za Mabawe, Mtobeye, Mbuba na Nyakisasa Polisi hutoa huduma kupitia Vituo Maalum vya Operesheni vya maeneo ya Murugyagira, Rulenge, Kabanga na Bugaramo. Hata hivyo, Serikali itajenga vituo vya polisi katika maeneo hayo kwa awamu kulingana na upatikanaji wa fedha.