Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 11 Sitting 41 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 342 2018-05-31

Name

Hassanali Mohamedali Ibrahim

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiembesamaki

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y MHE. IBRAHIM HASSANALI MOHAMMEDALI) aliuliza:-
Wananchi au taasisi zilizopewa vibali vya kupaki magari hadi saa 12 jioni katika Jiji la Dar es Salaam sasa wanatumia vibali hivyo kupaki kwa saa 24. Hali hiyo imeibua usumbufu kwa wananchi wanaotaka kupaki magari yao kuanzia saa 12 jioni:-
Je, ni lini Serikali itakomesha suala hilo ili kuwaondolea wananchi usumbufu wanaoupata?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH S. KANDEGE) alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassanali Mohamedali Ibrahimu, Mbunge wa Kiembe Samaki, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Sheria Ndogo ya Maegesho ya Magari katika Tangazo la Serikali (GN) Na. 60 la mwaka 1998 na marekebisho yake (GN) Na. 41 ya mwaka 2017, maegesho ya kulipia pamoja na maegesho yaliyohifadhiwa (Reserved Parking) yanapaswa kutumika kuanzia saa 2.00 asubuhi mpaka saa 12.00 jioni, baada ya muda huo maegesho yote yanatakiwa kuwa wazi kwa ajili ya matumizi ya umma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini ikiwemo Jiji la Dar es Salaam kusimamia vyema utekelezaji wa sheria hii na kuhakikisha chanzo hiki cha mapato kinasimamiwa ipasavyo ili halmashauri zinufaike na chanzo hiki.