Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 session 13 Sitting 1 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 08 2018-11-06

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha Mji Mkongwe wa Mikindani uliopo katika Manispaa ya Mtwara Mikindani unakuwa kivutio cha utalii?

Name

Constantine John Kanyasu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Issa Malapo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Wizara imeweka mkakati mahsusi wa kuendeleza Mji Mkongwe wa Mikindani na kuutangaza ndani na nje ya nchi kama kivutio cha utalii. Mwaka 2016 Wizara kupitia Idara ya Mambo ya Kale ilianzisha kituo kipya cha mambo ya kale ndani ya Mji wa Mikindani. Kwa kuanzia Wizara imepeleka watumishi wawili na itaendelea kuongeza idadi ya watumishi kadri upatikanaji utakavyokuwa. Kituo hicho kimelenga kusimamia uhifadhi na matumizi endelevu ya malikale zinazopatikana katika Mji Mkongwe wa Mikindani. Aidha, mwaka 2017 kupitia Tangazo la Serikali namba 308 Wizara ilitangaza mji huu kuwa urithi wa utamaduni wa Taifa. Mji Mkongwe wa Mikindani ni kati ya maeneo…