Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 1 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 3 2019-01-29

Name

Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. GIBSON B. MEISEYEKI aliuliza:-

Mheshimiwa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete aliahidi ujenzi wa barabara yenye urefu kwa kilomita 12 katika Jimbo la Arumeru Magharibi na sasa imepita miaka 10 bila kutekelezwa ahadi hiyo:-

Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza ahadi hiyo hasa ikitiliwa maanani kuwa katika Jimbo la Arumeru Magharibi hakuna barabara ya lami hata nusu kilomita?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Gibson Blasius Ole Meiseyeki, Mbunge wa Arumeru Maghari kama ifuatayo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete alitoa ahadi ya ujenzi wa barabara ya lami kilomita 12 Arumeru Magharibi mwezi Novemba, 2012 kwenye uzinduzi wa Hospital ya Wilaya ya Oltrumeti.

Mheshimiwa Spika, Serikali ilikwishaanza utekelezaji wa ahadi hiyo ya Mheshimiwa Rais Msaafu ambapo kati ya mwaka wa fedha 2014/2015 hadi 2017/2018 barabara zenye urefu wa kilomita 3.55 kwa kiwango cha lami zimejengwa Arumeru Magharibi kwa gharama ya shilingi bilioni mbili. Barabara zilizojengwa ni kama ifuatavyo: Mianzini-Timbolo kilomita 0.8; Sarawani-Oldonyosapuk kilomita 0.7; Tribunal Road kilomita 2.5; na Sekei-Olglai kilomita nne (4). Serikali itaendelea kutenga fedha za ujenzi wa barabara hizo kwa kiwango cha lami kwa kadiri fedha zinavyopatikana.