Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 11 2019-01-30

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ANNE K. MALECELA aliuliza:-

Barabara ya Hedaru – Vunta – Myamba Wilaya ya Same ni korofi sana na kusababisha usafiri wa barabara ya Tarafa ya Mamba/Vunta kuwa mgumu:-

Je, Serikali inawasaidiaje Wananchi wa Tarafa ya Mamba/Vunta ili waweze kuendelea kiuchumi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela, Mbunge wa Kuteuliwa kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Hedaru – Vunta – Myamba yenye urefu wa Kilometa 42.2 inahudumiwa na Wakala wa Barabara Vijijini na Mjini (TARURA), Wilaya ya Same. Barabara hiyo ipo Ukanda wa Milimani na uhalibifu wake hunatokana na changamoto ya maji ya mvua yanayosababisha maporomoko ya udongo na kuchimbika kwa barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mwaka wa Fedha 2018/2019, barabara hiyo ilitengewa kiasi cha shilingi Milioni 20 kwa ajili ya ujenzi wa mifereji ya maji ya mvua na vivuko viwili. Uwekaji wa Miundombinu hiyo utapunguza uharibifu unaotokana na maji ya mvua. Kazi hizo zinaendelea kutekelezwa. Kwenye Mpango wa Bajeti ya Mwaka wa Fedha 2019/2020, Serikali imeweka kipaumbele na kutenga jumla ya shilingi milioni 87.72 kwa ajili ya kuiwekea changarawe kwenye sehemu korofi.