Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 2 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 12 2019-01-30

Name

John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. JOHN W. HECHE aliuliza:-

Hospitali ya Wilaya ya Tarime imeelemewa na Wagonjwa kwa sababu inapokea Wagonjwa wengi kutoka Wilaya ya Tarime na Rorya, pamoja na uchache wa Vituo vya Afya, Zahanati na Vifaa katika maeneo mengi ya Wilaya hizo.

Je, ni kwa nini Serikali isipandishe hadhi Hospitali hiyo na kuwa Hospitali ya Mkoa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa John Wegesa Heche Mbunge wa Tarime Vijijini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi 367,985 wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wanapata huduma za afya katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime iliyoko Tarime Mjini pamoja na Vituo vya Afya vinane ambavyo vitano vinamilikiwa na Serikali na vitatu vinamilikiwa na Watu Binafsi na Zahanati 23 za Serikali zikiwa 16 na 7 Watu binafsi. Vilevile, Hospitali hiyo inahudumia wilaya za jirani ambazo ni Rorya, Musoma na Bunda na wagonjwa kutoka nchi jirani ya Kenya na kusababisha msongamano wa wagonjwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali haina mpango wa kupandisha hadhi Hospitali ya Wilaya ya Tarime kuwa Hospitali ya Mkoa kwa kuwa Mkoa wa Mara una Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara iliyoko Musoma Mjini. Ili kutatua changamoto ya utoaji wa huduma za Afya katika Mkoa wa Mara, Serikali katika Mwaka wa Fedha 2018/2019 imetenga kiasi cha shilingi bilioni 4.5 kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali tatu za halmashauri katika Halmashauri za Wilaya ya Bunda, Rorya na Musoma.

Tayari fedha zote zimepelekwa kwenye Halmashauri husika kwa ajili ya kuanza ujenzi. Vilevile, Serikali inaendelea na Ukarabati na ujenzi wa Vituo sita vya Afya katika Mkoa wa Mara vinavyogharimu jumla ya shilingi bilioni 2.4. Ujenzi wa Hospitali tatu za halmashauri na Vituo sita vya Afya utaimarisha huduma katika ngazi ya msingi na kupunguza msongamano wa Wagonjwa katika Hospitali ya Wilaya ya Tarime.