Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 6 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 53 2019-02-04

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA aliuliza:-

Halmashauri ya Geita DC ina Majimbo mawili ya Geita Viijini na Busanda ambayo kiutawala husababisha usumbufu na hali tete kwa wananchi kijiografia na mkoa ulishapitisha kuomba Serikali iigawe kuwa na Halmashauri ya Busanda:-

Je, ni lini Serikali itaridhia ombi hilo?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Kasheku Musukuma, Mbunge wa Geita Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa, Sura Na. 287 (Mamlaka za Wilaya) na Sura Na. 288 (Mamlaka za Miji) pamoja na Mwongozo wa Serikali kuhusu Uanzishaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wa Mwaka 2014, mapendekezo ya kuigawa Halmashauri yanapaswa kujadiliwa kwanza kwenye Kikao cha Baraza la Madiwani, Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) na Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) kisha kuwasilishwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa uamuzi.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Geita imeshajadili suala hili katika Kikao cha Baraza la Madiwani ingawa bado halijapelekwa kwenye Vikao vya Ushauri vya Wilaya (DCC) na Mkoa (RCC). Mara mchakato utakapokamilika na maombi kuletwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tathmini itafanywa na kuona kama kuna haja ya kuigawa Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Mheshimiwa Spika, aidha, kipaumbele cha Serikali ya Awamu ya Tano ni kuimarisha maeneo yaliyokuwa yameanzishwa ili yaweze kutoa huduma kwa wananchi kama ilivyokusudiwa badala ya kuendelea kuanzisha maeneo mapya ambayo hayaondoi kero ya kusogeza huduma kwa wananchi.