Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 8 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 94 2019-02-06

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza:-

Mji wa Itigi unakua kwa kasi na umeme umeenda vijiji vya Lulanga, Itagata, Ukimbu, Chabutwa, Mtakuja, Makale na Mitundu ambapo ni kilomita 71; kwenda Itigi hadi Mwamagembe ni zaidi ya kilomita 130:-

(a) Je, Serikali haioni ni vema sasa kuipa TANESCO hadhi ya Kiwilaya katika Wilaya ya Itigi?

(b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza watumishi wa Shirika la Umeme katika Jimbo la Manyoni Magharibi?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Omary Massare, Mbunge wa Manyoni Magharibi, lenye sehemu (a) na (b) kwa pamoja, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuleta ufanisi katika kuwahudumia wananchi wa Mji wa Itigi katika Jimbo la Manyoni Magharibi mwaka 2003 TANESCO ilianzisha Ofisi ndogo ya Itigi kwa lengo la kuongeza huduma za umeme kwa wananchi. Aidha, TANESCO imekuwa ikifungua ofisi kwa ajili ya kutoa huduma kwa wateja wake katika maeneo mbalimbali nchini. Vilevile Ofisi hizo zimekuwa zikipandishwa hadhi kutoka ofisi ndogo hadi kuwa Ofisi za Wilaya na Mkoa za TANESCO kwa kuzingatia mahitaji ikiwa pamoja na kukua kwa shughuli za uchumi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa TANESCO imefungua ofisi katika Mji wa Itigi kwa ajili ya kuwahudumia wateja katika hadhi ya ofisi ndogo. Hata hivyo, TANESCO imeanza taratibu za kupandisha ofisi hiyo hadhi ili kuwa ofisi ya TANESCO ya Kiwilaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya TANESCO Itigi inasimamiwa na Techinician na watumishi wengine 11. Katika mwaka wa fedha 2018/2019, TANESCO inatarajia kuongeza watumishi wengine watano pamoja na Mwandisi ili kuwahudumia wateja wa maeneo yote ya Itigi ikiwa ni pamoja na wateja kutoka Vijiji vya Lukanga, Itagata, Ukimbu, Chabutwa, Mtakigi, Makle, Mitundu na Mwamagembe.