Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 14 Sitting 10 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 122 2019-02-08

Name

Godbless Jonathan Lema

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arusha Mjini

Primary Question

MHE. GODBLESS J. LEMA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza kunufaika na nishati mbadala itokanayo na jua hasa, katika mikoa yenye ukame unaosababishwa na jua kali kwa kutengeneza Solar Village na kuunganisha nishati hiyo kwenye Gridi ya Taifa?

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Godbless Jonathan Lema, Mbunge wa Arusha Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TANESCO inatekeleza Mradi wa Nishati Endelevu kwa Wote (Sustainable Energy for all – SE4ALL) chini ya ufadhili wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).

Kazi zilizofanyika hadi kufikia Disemba, 2018 ni pamoja na uhakiki wa kubainisha sehemu zinazofaa kwa uzalishaji wa nishati ya umeme-jua katika maeneo ya Same (Kilimanjaro) Zuzu (Dodoma) na Manyoni (Singida). Ili kuwa na uhakika wa uwezo wa kuzalisha umeme katika maeneo hayo, Serikali kupitia TANESCO imeanza kufanya upembuzi yakinifu katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia TANESCO imeanza kutekeleza mradi wa kuzalisha umeme-jua wa MW 150 katika Wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga. Gharama ya mradi ni Dola za Marekani milioni 375.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mshauri Mwelekezi anatarajia kukamilisha upembuzi yakinifu mwezi Machi, 2019. Ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza mwezi Oktoba, 2019 na kukamilika mwezi Machi, 2021.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na utekelezaji wa miradi hii, Serikali kupitia TANESCO mwezi Oktoba, 2018, ilitangaza zabuni kwa ajili ya kupata wawekezaji binafsi watakaozalisha umeme. Kampuni 52 zimeonesha nia ya kuzalisha umeme kutoka chanzo hicho na hivi sasa, TANESCO wanafanya uchambuzi kwa ajili ya kupata Kampuni ya kuzalisha umeme MW 150 kutoka vyanzo mbalimbali vya nishati jadidifu pamoja na umeme wa jua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.