Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 1 Water and Irrigation Wizara ya Maji 1 2019-04-02

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. KISWAGA B. DESTERY aliuliza:-

Serikali ilikuwa na mpango wa kupeleka maji katika Mji wa Kisesa - Bujora na Kata ya Bukandwe:-

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga na kupeleka maji katika miji hiyo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiswaga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Uwekezaji ya Ulaya na Shirika la Maendeleo la Ufaransa inatekeleza Programu ya Majisafi na Usafi wa Mazingira katika Jiji la Mwanza na Miji ya Magu, Lamadi na Misungwi na miradi ya Majitaka katika Miji ya Bukoba na Musoma kwa gharama ya EURO million 104.5.

Aidha, kupitia programu hii, AFD imeridhia kutoa fedha ya nyongeza (additional financing) kiasi cha EURO milioni 30 sawa na shilingi bilioni 75 kwa masharti ya mkopo nafuu. Kwa sasa mchakato wa kutia saini Mkataba wa Makubaliano ya Kifedha (Financing Agreement) kati ya AFD na Wizara ya Fedha na Mipango unaendelea.

Mheshimiwa Spika, kulingana na andiko la mradi, fedha hizo za nyongeza zitatumika kutekeleza mradi wa kupeleka maji katika maeneo ya Usagara, Buhongwa, Busweru na Mji mdogo wa Kisesa - Bujora na Kata ya Bukandwe pamoja na Vijiji vya Igetimaji, Kitumba, Mwahuli, Busekwa na Ihayabuyaga. Mradi huu unategemewa kuanza katika mwaka wa fedha 2019/2020.

Hivyo, nawaomba wananchi wa Kisesa, Bujora na Kata ya Bukandwe wawe na subira kwa kuwa mpango wa kuwapelekea maji uko katika hatua nzuri.