Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 1 Water and Irrigation Wizara ya Maji 2 2019-04-02

Name

Dr. Jasmine Tiisekwa Bunga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Vyuo Vikuu

Primary Question

MHE. DKT. JASMINE T. BUNGA aliuliza:-

Kumekuwepo na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi dhidi ya Mamlaka za Maji Safi katika Halmashauri mbalimbali kwa kuwapatia wananchi bili kubwa za maji ambazo haziendani na uhalisia:-

Je, ni lini Serikali itaanzisha utaratibu wa kulipia maji kadri utumiavyo katika utoaji wa huduma hiyo kama ilivyo kwenye umeme?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Jasmine Tisekwa Bunga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali imeshaanza kutumia utaratibu wa kulipa maji kadri unavyotumia (pre-paid meters) katika maeneo mbalimbali nchini. Kwa sasa utaratibu huo umeanza kutumika katika maeneo yanayohudumiwa na Mamlaka za Arusha, Iringa, Songea, Dodoma, Tanga, Mbeya, Tabora, Mwanza, Moshi na DAWASA.

Mheshimiwa Spika, Serikali imeagiza Mamlaka zote nchini kuendelea kuwafungia wananchi dira za maji za kulipa maji kadri watumiavyo ili kupunguza malalamiko ya wananchi pamoja na kupunguza tatizo la malimbikizo ya madeni ya matumizi ya maji.