Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 3 Water and Irrigation Wizara ya Maji 21 2019-04-04

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE aliuliza:-

Baada ya Serikali kukamilisha usanifu wa mradi wa maji wa vijiji 57 kwenye kata 15 Wilayani Kyerwa:-

Je, Serikali ipo tayari kutenga fedha kwenye Bajeti ya 2019/2020 ili miradi hiyo ianze kutekeleza Ilani ya CCM ya kumtua mama ndoo kichwani?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mradi wa vijiji 57 kwenye kata 15, Wilayani Kyerwa ni miongoni mwa miradi mikubwa ya maji ambayo Serikali ina mpango wa kuitekeleza ili kuhudumia wananchi wengi. Mradi huu unalenga kuhudumia watu takriban 282,000 waishio kwenye vijiji hivyo utakapokamilika.

Mheshimiwa Spika, usanifu wa mradi huu umekamilika na imeonekana kuhitaji kiasi kikubwa cha fedha. Hivyo, Serikali inafanya jitihada za kutafuta fedha za kutekeleza mradi huu wa kimkakati (Strategic Water Project).