Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 6 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 49 2019-04-09

Name

Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SONIA J. MAGOGO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wananchi wa Wilaya ya Handeni ambao wanakosa ardhi ya kuendesha shughuli zao za kilimo kwa sababu ya kumilikiwa na wachache?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sonia Jumaa Magogo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukaguzi wa mashamba uliofanyika katika kipindi cha 2018/2019 Wilayani Handeni ulibaini kuwepo kwa mashamba manne makubwa yenye hekta 7,279.26 ambayo hayajaendelezwa ipasavyo na hivyo kupelekea baadhi ya mashamba hayo kuvamiwa na wananchi. Serikali inaendelea na utaratibu wa ufutaji wa miliki za mashamba hayo yaliyokiuka masharti ya uendelezaji ambapo wamiliki wanne wameshatumiwa ilani zao ubatilisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya miliki hizo kubatilishwa, ardhi husika itaandaliwa mipango ya matumizi ikiwemo ya kilimo na ufugaji na kugawia kwa wananchi wenye uhaba wa ardhi. Aidha, mipango hiyo itazingatia utengaji wa ardhi ya akiba (land bank) kwa ajili ya matumizi ya baadaye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, natoa rai kwa wananchi kutumia ardhi yao kwa tija kwani ardhi haiongezeki wakati idadi ya watu, mifugo na shughuli za uzalishaji zinahitaji ardhi zinaongezeka. Vilevile, viongozi wa Vijiji na Kata waache tabia ya kuwagawia ardhi kwa mtindo wa kuwakodisha wananchi kwa kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha taratibu na sheria za nchi yetu.