Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 53 2019-04-10

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA (K.n.y. MHE. MENDRAD L. KIGOLA) aliuliza:-

Sekondari za Jimbo la Mufindi Kusini zinakabiliwa na tatizo la hosteli kwa ajili ya wanafunzi wanaotoka mbali:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga hosteli kwa kila sekondari katika Jimbo la Mufindi Kusini?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa
Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mendrad Lutengano Kigola, Mbunge wa Mufindi Kusini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi ina shule za sekondari 43 ambapo kati ya hizo shule 21 zina daharia (hostel). Katika mwaka wa fedha 2018/2019, shule nyingine mbili za sekondari za Ihowanza na Mninga zinaendelea na ukamilishaji wa ujenzi wa hosteli ili kufanya idadi ya shule zenye hosteli kufikia 23.

Aidha, kwa mwaka wa fedha 2019/2020, Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi imetenga kiasi cha shilingi milioni 60 kupitia mapato ya ndani ili kusaidia ukamilishaji wa daharia zilizopo katika hatua ya ukamilishaji. Vilevile Lyara in Africa wamepanga kusaidia ujenzi wa hosteli katika Shule za Sekondari za Kiyowela na Idunda na CAMFED wamesaidia ujenzi wa hosteil ya Ihowanza.