Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 15 Sitting 7 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 54 2019-04-10

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE aliuliza:-

Wanawake Mkoani Kigoma wameitikia wito wa kujiunga katika vikundi vya ujasiriamali kama vile vikundi vya kilimo cha muhogo, kurina na kuchakata asali na VICOBA:-

Je, Halmashauri za Wilaya za Mkoa wa Kigoma zimechangia kiasi gani kwa vikundi hivyo kama sheria inavyotamka?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Josephine Johnson Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2017/2018, Halmashauri za Mkoa wa Kigoma zilitoa shilingi milioni 250 kwa ajili ya vikundi vya wanawake na vijana. Kati ya fedha hizo, shilingi milioni 129 zilitolewa kwa vikundi vya wanawake. Aidha, katika mwaka wa fedha 2018/2019 hadi Februari 2019, Mkoa wa Kigoma umetoa shilingi milioni 249 kwa ajili ya vikundi 171 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu. Kati ya fedha hizo shilingi milioni 181 zimetolewa kwa vikundi 120 vya wanawake.

Mheshimiwa Naibu Spika, Ofisi ya Rais - TAMISEMI itaendelea kusimamia sheria inayozitaka Halmashauri kutenga, kutoa mikopo na kusimamia marejesho ya fedha hizo kutoka kwenye vikundi vilivyonufaika. Ahsante.